Habari
Serikali ya Tanzania kuburuzwa mahakamani, yapewa siku 45 kujibu malalamiko ya wapinzani (+video)
Serikali ya Tanzania imepewa siku 45 za kujibu malalamiko ya vyama 8 vya upinzani yaliyopelekwa katika Mahakama ya Afrika Mashariki, juu ya kupinga Sheria mpya ya Vyama vya Siasa.
Kesi hiyo imesajiliwa kwa namba 3/2019, na imefunguliwa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mhe. Freeman Mbowe na wenzake wanne.