Habari
Serikali ya Wanafunzi UDSM yatoa saa 72 kwa Bodi ya Mikopo (HESLB) kutekeleza maagizo haya manne
Serikali ya Wanafunzi UDSM yatoa saa 72 kwa Bodi ya Mikopo (HESLB) kutekeleza maagizo haya manne
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam wametishia kwenda kukusanyika katika Ofisi ya Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu, (HELSB), endapo ndani ya saa 72 watakuwa hawajawaingizia fedha baadhi ya wanafunzi ambao ni wanufaika wa mkopo.
Maazimio ya wanafunzi wa UDSM dhidi ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu. DARUSO imetoa saa 72, bodi iwe:
i. Imepeleka fedha za wanafunzi chuoni
ii. Imerudisha fedha za wanafunzi zilizokatwa
iii. Imewapangia mikopo waliokata rufaa
iv. Imbadili afisa mikopo chuoni hapo
By Ally Juma.