Habari

Serikali yaweka wazi hali ya uchumi wa nchi

Serikali kupitia Msemaji Mkuu wake, Dkt. Hassan Abbas imesema kuwa kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Fedha Duniani (IMF) inaonyesha uchumi wa nchi uko imara ukilinganisha na nchi zilizofanyiwa tathimini.


Mkurugenzi wa Idara ya habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbas akizungumza na waandishiwa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelelezo uliopo jengo la LAPF mjini Dodoma

Dkt. Abbasi ameyasema hayo mjini Dodoma alipokuwa akiongea na waandishi wa habari juu ya maoni ya wataalam wa uchumi kutoka IMF ambao wamemaliza ziara yao hapa nchini Desemba 12, 2017.

“Ripoti ya IMF inaonesha katika nusu ya kwanza ya mwaka 2017 uchumi umekua kwa asilimia 6.8, takwimu ambazo ni za juu katika chumi zinazokua kwa kasi na ikizidi nchi kadhaa zilizofanyiwa tathmini mwaka 2017 zikiwemo za Ulaya,” amesema Dkt. Abbas.

Aidha, kutokana na usambazaji mzuri wa chakula mfumuko wa bei ya chakula ulishuka hadi kufikia asilimia 4.4 ikiwa ni chini ya lengo ambalo IMF ilitabiri mfumuko ungekuwa asilimia 5.

Aidha amesema, Serikali imeendelea kulipa madeni ya ndani ambapo mpaka sasa Shilingi bilioni 900 zimeshalipwa na shilingi bilioni 37 zimelipa madeni ya watumishi wa Serikali.

Timu hiyo ya wataalamu kutoka IMF iliongozwa na Bw. Mauricio Villafuerte ambapo walifanya ziara juu ya tathimini ya uchumi katika nchi Saba Afrika ikiwemo Tanzania pamoja na Msumbiji, Rwanda, Nigeria, Uganda, Senegari na Cape Verde.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents