Michezo
Sevilla itaendelea na mfumo wa kushambulia – Eduardo
Kocha mpya wa klabu ya Sevilla ya nchini Hispania, Eduardo Berizzo amesema ataendeleza mfumo wa kushambulia ambao umeachwa na meneja Jorge Sampaoli.
Kocha wa klabu ya Sevilla ya nchini Hispania, Eduardo Berizzo
Sampaoli alikinoa kikosi hicho na kukiwezesha kumaliza katika nafasi ya nne msimu uliomalizika kabla ya kwenda kuitumikia timu ya Taifa ya Argentina.
Meneja huyo wa zamani wa Celta Vigo, Berizzo alithibitisha falsafa ya Sampoli ataiendeleza ndani ya kikosi hicho ambacho kilifanya vyema zaidi msimu wa mwaka 2016/17
BY HAMZA FUMO