Shaggy akiwasili Zenji
MWANAMUZKI wa Kimataifa Shaggy leo amewasili saa 9: 30 Zanzibar akitokea Dar es salaam kwa Boti ya kukodiwa baada ya kukataa kupanda ndege kwa lengo la kutumia boti katika safari yake hiyo ya kuja Zanzibar katika Tamasha la Filamu Zanzibar ‘ZIFF’.
Inasemekana mwanamuziki huyo alitoka Dar es salaam tangu saa 7 mchana na kuwasili Zanzibar saa 9 na nusu, kwa kutumia boti ya kukodi huku akitumia muda mwingi baharini.
Shaggy anatarajiwa leo kufanya Show katika ukumbi wa Ngome Kongwe, katika usiku wa leo yaani Ijumaa kuamkia Jumamosi kwaajili ya Tamasha la Filamu la Zanzibar ‘ZIFF’
Mwanamuziki Shaggy akipanda kwenye ngazi kutoka kwenye boti iliyomfikisha Zanzibar kutoka Dar.
Boti ndogo ambayo ilienda kumpokea na kumleta hadi kando kando ya bustani ya Forodhani iliyopo mbele ya Jumba la Kome Kongwe.
Shaggy akiingia Zenji
Hapa wananchi wakimpokea na walinzi wakimpeleka sehemu nzuri kwaajili ya mapumziko ya muda.
Shaggy akipiga saruti ya vidole viwili kuwasalimia mashabiki wake ambao wamekuwa wakishangilia tangu kushuka kwake kwenye Boti
Warembo wa Tusker , wakijiandaa kumpokea Shaggy ambaye alikuwa tayari ameshakaribia.
Wavuvi wakiwa karibu na mitubwi yao wakimwangalia Shaggy akiwasili.
Msafara wa Shaggy akitoka maeneo ya Bustani ya Forodhan, na kwenda sehemu ya kupumzika kwa muda na kisha baadaye arudi kwaajili ya Tamasha lenyewe la Visiwa vya karafuu, ZIFF.
Wafanya kazi wa Radio ya Coconut ‘Fm, ambayo ndiyo waliomleta Shaggy katika tamasha filamu Zanzibar ZIFF.