Habari

Sheikh Ponda ajisalimisha Polisi

Baada ya hapo jana Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kumtoka Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda kuripoti kituoni hapo ndani ya siku tatu hatimaye amefanya hivyo.

Katika mkutano na waandishi wa habari Kamishna wa Kanda hiyo, SACP Lazaro Mambosasa alimtaka Sheikh Ponda kufika kituo cha Polisi kwa tuhuma za uchochezi na kuikejeli Serikali ambazo alitoa hivika karibuni.

Kauli hizo zinadai Sheikh Ponda alizitoa October 11 mwaka huu katika mkutano na waandishi wa habari ambapo inaharifiwa kuwa Polisi baada ya kupata taarifa za uwepo wa mkutano huo walifika eneo la tukio lakini hawakufanikiwa kumapata Sheikh Ponda.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents