Burudani
Shetta akanusha kubebwa kwenye kolabo anazofanya
Hitmaker wa Shikorobo, Shetta amekanusha kubebwa na wasanii anaofanya nao kolabo na kwamba nyimbo anazofanya mwenyewe hazifanyi vizuri.
Shetta ameiambia Bongo5 kuwa nyimbo zake nyingi alizowashirikisha wasanii wengine yeye ndio amekuwa akifanya kazi kubwa.
“Mimi naamini ngoma kama Shikorobo nimeimba chorus mwenyewe na verse mbili mwenyewe,” amesema. “Ningekuwa nimemtoa pia ningefanya vizuri. Kcee amekuwepo kwa sababu ni international artist ili kufanya kubwa zaidi Nigeria, pia yeye anakuhitaji huku na mimi nakuhitaji kule. Kwahiyo amenitumia mimi na mimi nimemtumia yeye.”
“Maneno kama hayo hayaniumizagi as long as nafanya kazi nzuri na ngoma zangu nyingi kazi kubwa nafanya mimi,” amesisitiza.