Burudani
Shetta: Nina ngoma saba mpya na zote kali
Baada ya Shikirobo tarajia ngoma zingine kali kutoka kwa Shetta.
Rapper huyo ameiambia Bongo5 kuwa ameandaa nyimbo saba mpya ambapo atachagua moja ya kutoka. Amesema muziki wa sasa unahitaji nyimbo nzuri na sio kubahatisha.
“Watu wategemee ngoma kali, sitaki kuongea sana, video kali. Kuna ngoma kama saba nimeziandaa,” amesema Shetta.
“Yeyote itatoka kwasababu muziki umekuwa unahitaji kazi nzuri ili iweze kufanya vizuri. Kwahiyo naweza nikatoa collabo pia, chochote kinaweza kutokea.”