Bongo Movie

Shilole aeleza kwanini mgahawa wake ameupa jina ‘Trump Food’ (Video)

Msanii wa muziki na filamu Shilole amefungua mgahawa wake mpya Kinondoni jijini Dar es saalam na kuupa jina ‘Trump Food’.

Akizungumza na Bongo5 wiki hii, Shilole amedai amelipenda jina hilo kwa kuwa yeye anapenda harakati za Rais wa Marekani Donald Trump.

“Mgahawa unaitwa ‘Trump Food’ kwa sabubu Shishi kama Shishi ni super woman, Trump hana shobo na mtu, akitaka kufanya kitu anafanya kama mimi nafanya na naendelea kufanya, kwa hiyo aim Trump baby,” alisema Shilole.

Muimbaji huyo alisema toka aufungue mgahawa huyo mambo yanaenda vizuri.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents