Burudani
Shilole: Collabo yangu ya Wizkid na Koffi zinakuja, wameniambia niende nchini kwao kwanza (+Video)
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva @officialshilole amezungumzia suala la yeye kufanya Collabo na @wizkidayo pamoja na @koffiolomide_officiel
@officialshilole ameongeza kuwa ingawa alipata shida sana kuongea na uongozi wa @wizkidayo lakini kwa sababu meneja wa @wizkidayo Sunday anamkubali sana hivyo wameelewana atasafiri kwenda Nigeria kwa ajili ya kurekodi.
Kuhusu Collabo na @koffiolomide_officiel ameeleza kuwa mipango tayari imekamilika na pia atasafiri kwenye Congo kwa ajili ya kurekodi kwenye studio ya Mopao na kushot video kwenye hotel yake huko Kinshasa.