Burudani
Show za Ulaya zamweka busy Bizman
Msanii wa muziki na mtayarishaji wa muziki aliyewahi kufanya kazi na watayarishaji wakubwa wakiwemo P-Funk na Master J amesema ukimya wake umetokana na ziara za Ulaya za bendi yake ya In Africa Band.
Bizman akiwa na In Afrika Band
Akizungumza na Planet Bongo, Bizman alisema amekuwa akisafiri na kufanya show katika mataifa mbalimbali.
“Sasa hivi nipo Bongo mpaka December. Hivi ndio natarajia kwenda kwenye ziara zetu za Ulaya nikiwa na In Africa Band,” alisema.
“Ukimya wangu mwingi ni kutokana In africa Band, kwahiyo muda mwingi ninakuwa nje ya nchi. Ila kwa sasa nipo mpaka December kwahiyo wakihitaji sasa hivi nipo,” alisema.