Burudani

Sijapewa zawadi zangu mpaka leo – Miss Tanzania 2016 (Diana Edward)

Baada ya kufanikiwa kulinyakua taji la Miss Tanzania 2016/2017 na kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kumtafuta mrembo wa dunia huko nchini Marekani mwishoni mwa mwaka jana, mrembo Diana Edward amesema kwamba mpaka sasa bado hajamaliziwa kupewa zawadi zake.

Mrembo huyo mwenye asili ya kimasai kutoka Arusha amefunguka hayo nilipoongea naye exclusively hivi karibuni kwa kudai kuwa hajapewa zawadi zake mpaka leo ikiwemo gari na kiasi fulani cha fedha na ndio yupo anafuatilia kwa sasa.

Diana alimalizia kwa kusema kuwa kwa sasa inamlazimu kutumia tax na bodaboda kufanyia mizunguko yake ya kila siku .

Msikilize Diana hapo juu.

Na Edward Fabian

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents