Habari
Sikiliza sauti ya kilichotokea wakati trafiki alipomsimamia mke wa waziri na kupelekea kupandishwa cheo
Hakuna aliye juu ya sheria. Mke wa waziri (jina kapuni) ameligundua hili kwa njia ya kufedhehesha zaidi.
Mama huyo alidaiwa kusimamisha gari kwenye alama za zebra na kumfanya trafiki amkamate. Baada ya kukamatwa mama huyo alidaiwa kuleta zile za ‘unajua mimi ni nani’, ‘unajua mimi ni mke wa waziri’ kumtishia trafiki huyo ambaye hakutishika.
Badala yake alimpigia simu bosi wake kumweleza kilichotokea. Juzi Rais Dkt John Magufuli alimwagiza IGP ampandishe cheo. Sikiliza sauti ya ilivyokuwa hapo chini.