Muziki
Sikiliza wimbo wa chipukizi huyu hapa, awataja Alikiba, Diamond, Wolper na Ommy Dimpoz
Mwaka 2018 umeanza vizuri kwa baadhi ya wasanii wapya katika tasnia ya muziki wa Bongo Flava kwa kuachia ngoma zao mpya kuonyesha uwezo wao.
Pasco Dee ni miongoni mwa chipukizi hao ambao wameuanza mwaka vizuri kwa ngoma zao kusikika kwa mara ya kwanza. Msanii huyo ameachia wimbo wake huo mpya ambao amefanya peke yake uitwao ‘Fake’.
Katika wimbo huo Pasco ameonekana kuwataja mastaa kibao wa Bongo Flava akiwemo Alikiba, Diamond, Wolper, Jokate, Ben Pol, Ommy Dimpoz na wengine.
Usikilize wimbo huo hapa chini.