Habari

Siku nikiletewa Muswada wa Habari nitausaini muda huo huo – Rais Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amesema siku akiletewa Muswada wa Sheria ya Vyombo vya Habari atausaini muda huo huo ili uanze kufanya kazi mara moja.

14592151_1674286826216648_4785838292216053760_n

Akizungumza katika mahojiano na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar es salaam, Rais Magufuli amesema hawezi kuzungumza lolote kuhusu muswada huo kwa kuwa muswada huyo utajadiliwa bungeni na wabunge wote.

“Kuniambia mambo ya bunge ambayo bado sijaletewa, utakuwa unanionea katika utawala wa bunge,” Magufuli alimjibu mwandishi aliyehoji kuhusu muswada huo. “Tuwaache wabunge watimize wajibu wao. Sasa unaponiambia ukiletwa niikatae nataka nikueleze bila unafiki siku utakapo fika siku hiyo hiyo nitausaini, ili msubiri kama utakuja wakati mwingine mje muubadilishe, sitaki kufrastuate mambo ya bunge,”

Aliongeza, “Lakini lazima tukubali kwamba hii sheria imechelewa, na unakuta mnazungumza kwa lugha ya wamiliki fulani fulani. Lakini muswada huu sifahamu wabunge watakacho amua lakini niya ni kulinda waandishi wa habari,”

14717590_1857398554483289_764705840287449088_n

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amewataka watanzania kufanya kazi kwa bidii ili wapate kipato kutokana na kazi wanazofanya.

“Tanzania ni tajiri, kinachotakiwa ni namna ya kubalance rasilimali, katika kufanya hilo mimi nimeamua kubana matumizi serikalini kwa mfano nimedhibiti safari za nje kwa kuanza na mimi mwenyewe, tangu niingie madarakani nimepata mialiko 47 lakini nimekwenda mialiko mitatu.” Alisema Rais Magufuli.

BY: EMMY MWAIPOPO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents