Habari
Siku ya Mazingira Duniani: Miss Ubungo Diana Kato afanya usafi hospitali ya Amana (+picha)
Aliyekuwa Miss Ubungo mwaka 2014-2016 Diana Joachim Kato ameshiriki katika kuadhimisha wiki ya mazingira iliyoanza Mei 31 hadi Juni 5, kwa kufanya usafi katika Hospitali ya Rufaa ya Amana jijini Dar es Salaam.
Aliyekuwa Miss Ubungo Diana Kato (Kushoto) akifuatiwa na Diwani wa kata ya Ilala, Saady Khimji
Mrembo huyo ambaye pia anamiliki mradi wa maji safi na salama, amefanya usafi huo kwa kushirikiana na Diwani wa Kata ya Ilala, Saady Khimji. Mbali na kufanya usafi huo Dina amepanda miti katika hospitali hiyo.
Tazama picha zaidi hapa chini.