Michezo
Simba Day yafana: Mnyama ‘Simba SC’ amjeruhi Rayon Sports (+Picha)
Klabu ya Simba imenogesha sherehe ya Simba Day kwa kufanikiwa kuichakaza klabu ya Rayon Sports FC kutoka Rwanda kwa bao 1-0 katika mechi ya kirafiki iliyofanyikia kwenye uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam jioni ya leo.
Bao la ushindi la Simba SC limefungwa na Mohamed Ibrahimu kunako dakika 15 za kipindi cha kwanza cha mpambano huo ambao Rayon Sports FC walionekana kuelemewa kwa kiasi kikubwa.
Tazama picha za Matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye mechi hiyo katika kuadhimisha siku ya klabu hiyo (Simba Day)