Michezo

Simba SC ilinyimwa penati mechi ya Mbao FC – Osman Kazi

Mwamuzi mkongwe mwenye beji ya FIFA nchini, Osman Kazi amesema kuwa Simba SC ilinyimwa penati ya wazi wakati wa mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Mbao FC uliyopigwa uwanja wa Taifa licha ya vijana hao kuibuka na ushindi wa mabao 5 – 0.

Mwamuzi Osman Kazi akichambua marudio ya michezo iliyopita

Kazi ambaye ni mwamuzi mstaafu na mwenye heshima kubwa nchini kufuatia kutenda vema kazi yake awapo uwanjani ameyasema hayo hapo jana kupitia luninga ya Azam tv.

Emmanuel Okwi alikuwa na mpira na anapo ingia nao eneo la goli, Ndikumana hajaugusa ule mpira bali mguu wake umeukwatua mguu wa kulia wa Okwi.

Kwa hiyo hii ilikuwa penati ya wazi kabisa, mwamuzi alikuwa karibu kabisa na eneo la tukio wala hakuitaji usaidizi wowote ila aliwanyima tu penati.

Mwamuzi Osman Kazi akiwa na rais mstaafu Jakaya Kikwete uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam

Katika mchezo huo Simba SC iliibuka na ushindi wa mabao 5 – 0 dhidi ya Mbao FC huku beki wao Yusuph Ndikumana akitolewa kwa kadi nyekundu.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents