Michezo
Simba SC yatoa baraka zote kwa Ndemla kutua Sweden
Klabu ya soka ya Simba imetangaza kuwa kiungo wake, Said Hamisi Juma (Ndemla) amepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa nchini Sweden.
“Ndemla amepata nafasi hiyo katika klabu ya AFC Eskilstuna inayoshiriki ligi kuu.” Imesema taarifa kutoka katika klabu ya Simba.
“Aidha Ndemla atakuwa katika majaribio hayo kwa siku 14 na anatarajia kuondoka nchini kesho.”