Michezo

Simba SC yatoa mchezaji bora wa VPL kwa mwezi Januari, 2018

Klabu ya Simba imetoa mchezaji bora wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara kwa mwezi Januari, 2018 ambapo mshambuliaji wake, John Bocco ametajwa kuwa ndiye mchezaji bora kwa mwezi huo.

 

Bocco amewashinda wachezaji wenzake akina Emmanuel Okwi na Awesu Awesu wa Mwadui kutokana na uchambuzi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za VPL.

Kwa mwezi Januari, Bocco ameisaidia Simba kupata pointi 9 katika michezo mitatu aliyocheza na kuendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi, huku akifunga mabao matatu na kutoa pasi mbili za usaidizi wa mabao.

Mshambuliaji huyo aliyesajiliwa na Simba msimu huu amecheza dakika zote 270 za michezo mitatu ya Simba mwezi Januari huku akionesha kiwango kikubwa katika kila mchezo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents