MichezoUncategorized

Simba yaingia mkataba wa mamilioni na MO ENERGY

Uongozi wa klabu ya Simba umetangaza kuingia mkataba wa mwaka na Kampuni ya Utengenezaji vinywaji ya A One Products kupitia kinywaji cha Mo Energy Drink.

Mkataba huo utakuwa na thamani ya fedha za kitanzania, shilingi milioni 250. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Mwasala Masoud amesema fedha hizo zitahusika na Simba kwa ajili ya shughuli mbalimbali ndani ya klabu.

Mwasala ameeleza kuwa kinywaji cha Mo Energy kitakuwa kinaiwakilisha kampuni ya A One kutokana na utengenezaji wa bidhaa zake ambazo inazalisha. Aidha, Mwasala ameeleza kuwa mkataba huo unaweza ukaongezwa tena baada ya kufikia ukingoni baada ya miezi 12 ijayo kumalizkika.

Baada ya A One na Simba kusaini mkataba huo, Kaimu wa Rais wa klabu hiyo, Salim Abdallah ‘Try Again, amesema fedha hizo ambazo ni milioni 250 zitaenda katika mradi wa ujezi wa Uwanja Bunju.

Ikumbukwe Simba walianzisha mradi wa ujenzi wa Uwanja huo lakini baadaye ukaja ukasimama kutokana na sakata la viongozi wa klabu akiwemo Rais Evans Aveva kushitakiwa mahakami.

Related Articles

One Comment

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents