Uncategorized
Simba yamtangaza mgeni rasmi kwenye mchezo wao dhidi ya JS Saoura michuano ya CAF Champions League
Mabingwa wa ligi kuu na wawakilishi wa Tanzania Simba SC wamethibitis ha kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson kuwa mgeni rasmi katika mchezo wao wa klabu bingwa dhidi ya JS Saoura.
Simba itashuka dimbani siku ya Jumamosi ya Januari 12 kuvaana na Waalgeria hao ikiwa ni mchezo wa kundi D lenye timu za Al Ahly ya Misri na AS Vita Club ya Congo.