Michezo
Simon Msuva,Abdulrahman Mussa washinda kiatu cha dhahabu
Baada ya kufanya vizuri msimu huu, Washambuliaji wawili Abdulrahman Mussa wa Ruvu Shooting na Saimon Msuva wa Yanga wameibuka na tuzo ya wafungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa 2016/17 iliyomalizika wikiendi iliyopita.
Kutokana na wachezaji hao kufungana Idadi sawa ya magoli (14) wamepewa zawadi sawa ya ufungaji bora ambapo watapata Shilingi Milioni 5.8 za kitanzania.
Kwa kuwa vijana wetu Abrahman Mussa na Simon Msuva VPL wamefunga mabao sawa 14 wote ni wafungaji bora na watapewa zawadi sawa @Tsh 5.8m
— Jamal Malinzi (@jamalmalinzi) May 22, 2017
Sherehe za ugawaji wa tuzo hizo za Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2016/17 zitafanyika kesho kutwa (Mei 24 mwaka huu) kwenye ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.