Sina ujauzito – Anita Joseph
Muigizaji wa filamu kutoka Nollywood -Nigeria, Anita Joseph, ambaye alitengeneza vichwa vya habari kwa muda kuwa ana ujauzito ameamua kuweka mambo sawa.
Anita Joseph
Anita ameamua kuweka hali ya hewa sawa kutokana na uzushi huo ulioanza kuzagaa katika mitandao ambapo aliposti vipimo katika ukurasa wake wa Instagram vilivyoonesha kuwa ana ujauzito.
Kwa mujibu wa muigizaji huyo ameeleza kuwa vipimo hivyo alivyopost ni vya rafiki yake wa karibu anayeishi USA, ambaye hakubahatika kupata mtoto kwa miaka 19 ya ndoa yake na hatimaye amefanikiwa kupata ujauzito.
“Sina ujauzito, ni picha za rafiki yangu wa karibu ambaye ni mjamzito , niliweka ile picha kutokana na kuwa kwa muda wa miaka 19 ya ndoa yake hakupata mtoto, hivyo nikaguswa sana na ndio maana nikapost” amesema Anita.
Pia Anita amesisitiza kuwa aliwahi kuoteshwa kuwa rafiki yake huyo ana watoto mapacha.
‘Nilimwambia kuwa nimeota una watoto mapacha, baada ya hapo nikawa na muombea kwa mungu ili afanikiwe na hatimaye baada ya miezi sita akanijulisha kuwa ni mjamzito ndiyo maana nikaguswa sana” amesimulia Anita
Na Laila Sued