Mitindo

Sio Bongo hata mbele Red Carpet inawasumbua

Hello mambo vipi ni mwaka mwingine tunakutana tena hapa katika habari mbalimbali za mitindo zinazofanya vizuri, na leo tutatazama ugonjwa unao anza kukua kila siku katika event zetu.

Watu wengi wanashindwa kuvaa vyema wawapo katika zuria jekundu ama red carpet hii ni kwakuwa kila mtu anaamini ana uwezo wa kujibunia nguo ama kujichagulia ni vazi gani alivae sehemu hiyo, Jambo ambalo linaweza kukuharibia the all event.


Kama unataka kupendeza na ku -look good kwenye event make sure unawaona wabunifu yani watu wanaojua vyema masuala ya mavazi na mambo mengine ikiwezekana ajiri mtu ambaye ataweza kukuweka vizuri katika mitoko yako.

Miaka kadhaa Tanzania kulikuwa na tatizo la watu kuchemka katika event lakini kadri siku zinavyokwenda watu wanazidi kuelimika, hii ni kutokana na kuongezeka kwa wabunifu na watu wanaojua masuala ya mitindoa ambo kazi yao kubwa ni kukujunza na kukufunza namna ya kuvaa katika masherehe mbalimbali.

Nini cha kufanya:
1. Ili tabia hii isikuwe hakikisha unakuwa na wabunifu na watu wanaoelewa vyema trending ya muda husika wakusaidie katika mitoko yako.
2. Penda kujua mwili wako ni namna gani. Mfano: Kama mwili wakoni mkubwa jua aina ya mavazi unayotakiwa kuvaa kama ni mdoago pia jua , vile vile kama unarangi ya kungaa ama una rangi ya mtu mweusi ni vizuri ukajua kitambaa kinachokufaa.
3. Sio lazima uende na muda wa aina ya mitindo ili upendeze jua nini unataka.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents