Burudani
Siumizwi tena na uzushi kuwa nabwia unga – Young Dee
Rapper Young Dee amesema haumizwi tena na uzushi wa watu kuwa bado anaendelea kutumia madawa ya kulevya.
Young Dee ameiambia Bongo5 kuwa, hawezi kuwazuia watu wanaoendelea kumsema anatumia madawa ya kulevya.
“Sasa hivi hainiumizi tena, hata mimi nashindwa kuelewa kwa nini watu wanaendelea kuniuliza kwanini natumia madawa. Ila mimi tayari nilishakanusha na walio wengi walielewa,” alisema Young Dee.