Habari

Size 8 ajitoa kwenye tuzo za Kisima

Muimbaji wa kike wa nchini Kenya Size 8 amekuwa msanii wa tatu kutangaza kujiondoa kwenye tuzo za Kisima baada DNA na Daddy Owen kutangaza wiki iliyopita.

Size 8 amedai kuwa hakuwa ameomba kushiriki kwenye tuzo hizo na alishangazwa kusikia kuwa ametajwa.

Muimbaji huyo alitajwa kuwania kipengele cha Boomba Song of the Year na wimbo wake Fire.

Pia msanii mwingine mwenye makazi yake Mombasa, Cannibal naye amewalalamikia waandaaji kwa kutaja wimbo wake wa zamani My Fans kuwania tuzo hizo wakati tayari ana nyimbo nyingine kama My City, My Town na Legend.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents