BurudaniHabari

Soggy Doggy kufunga ndoa April

Msanii wa miondoko ya Bongo Flava..Soggy Doggy,atatangaza rasmi kuachana na ukapera ktk siku au tuseme miezi michache ijayo kuanzia leo.

Msanii wa miondoko ya Bongo Flava..Soggy Doggy,atatangaza rasmi kuachana na ukapera ktk siku au tuseme miezi michache ijayo kuanzia leo.

Hayo yalithibitishwa na Soggy mwenyewe akiwa ndani ya ofisi zetu ambapo alipenda kuwataarifu wapenzi wa muziki wake kuwa..endapo mungu akipenda na mambo yakienda kama yalivyopangwa…basi Inshalah mwezi wa nne atauaga ukapera rasmi kwa kufunga ndoa mtoto mzuri aliyemtaja kwa moja tu la Bi S…*** !!!!

Kijana Soggy kwa kweli inaonekana ameamua kutuliza akili kwa kutulia na kuweka mtoto ndani..watakayeishi pamoja na kusaidiana kwa kila jambo kama dini zetu zinavyosema…kwa mantiki hiyo basi timu nzima ya DHW inamtakia Soggy kila lakheri ktk maandalizi ya harusi hiyo inayotarajiwa kuwa ya kufana.

Wasanii waliooa na kuolewa mpaka hivi sasa ni;

Lady Jay dee
Ray C
Luten Karama
Inspector Haroun
Spider
Mary G

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents