Habari
Soudy Brown, Maua Sama na Shaffih Dauda maombi yao ya dhamana kusikilizwa Jumatatu
Wakili wa Soudy Brown, Maua Sama, Shaffih Dauda na Michael Mlingwa amesema kuwa maombi ya dhamana dhidi ya wateja wake yatasikilizwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu siku ya Jumatatu Septemba 24, 2018 .
Wakili Jebra amethibitisha taarifa hizo, mapema leo baada ya wateja wake kushindwa kupelekwa mahakamani.
Soudy Brown, Maua Sama, Shaffih Dauda na wengineo walikamatwa wiki iliyopita kwa tuhuma mbali mbali na jeshi la polisi.
SOMA ZAIDI – Soudy Brown, Maua Sama, Mx , Shaffih Dauda na Luvanda waendelea kusota rumande