Burudani
Staa wa filamu za James Bond na Rachel Weisz watarajia kupata mtoto wa kwanza
Muigizaji Rachel Weisz amethibitisha kuwa wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza na Daniel Craig maarufu kama James Bond.
Mrembo huyo amethibitisha hilo wakati alipokuwa akiongea na New York Times. “I’ll be showing soon. Daniel and I are so happy. We’re going to have a little human. We can’t wait to meet him or her. It’s all such a mystery,” amesema Rachel.
Wawili hao walianza mahusiano Disemba 2010 na walifunga ndoa Juni 2011 huko mjini New York City, Marekani.
Wakati huo huo Rachel tayari ana mtoto mmoja wa kiume, Henry (11) ambaye amezaa na director wa Hollywood Darren Aronofsky, ambao walianza mahusiano mwaka hadi 2010.
Naye Daniel Craig amefanikiwa kupata mtoto mmoja anayeitwa Ella kutoka kwa aliyekuwa mkewe Fiona Loudon.