Habari

Staa wa SA aliyekuwa na tatizo na kukua haraka Ontlametse Phalatse afariki dunia

Staa wa nchini Afrika Kusini aliyekuwa akipendwa kutokana na kuwa mwenye furaha licha ya tatizo la kukua haraka alilokuwa nalo, Ontlametse Phalatse amefariki dunia.

Amefariki jana usiku kwenye hospitali ya Dr George Mukhari Academic huko Ga-Rankuwa, Pretoria. Phalatse aliyekuwa na miaka 18, alikuwa mmoja kati ya wasichana wawili tu nchini humo wenye tatizo hilo nadra liitwalo Progeria.

Awali madaktari wake walitabiri kuwa angekuwa hadi akifikisha miaka 14 tu. Mwezi uliopita Rais Jacob Zuma alitimiza ndoto ya msichana huyo kuonana naye.

Taarifa ya familia yake imesema: It is with great sadness to inform you of the passing of our first lady, Ontlametse Ntlami Phalatse. Our hearts are filled with pain and sadness but Ontlametse — as we know her — would want us to carry on with her courageous spirit.”

Alikuwa maarufu sana Instagram ambako alikuwa na followers 63.6k.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents