Stamina na Roma ‘ROSTAM’ wapiga show na mavazi ya viwandani jukwaani, wenyewe waeleza sababu ya kufanya hivyo (video+picha)
Rapper Roma Mkatoliki na Stamina (ROSTAM) jana waliitikisa Mbagala kwa kufanya bonge la show kwenye Ninogeshe Music Concert ambapo kitu cha kushangaza walipanda jukwaani wakiwa wamevalia mavazi ya viwandani.
Wakizungumza baada ya show hiyo, wawili hao wamedai kuwa wamevaa sare hizo za viwandani ili kuunga mkono sera ya Rais Magufuli ya Tanzania ya Viwanda.
“Wakati Mwingine Tunahisi kama Kiwanda Chetu Cha Burudani (Muziki Bongo Flavour) Hakitolewi Macho Na Kupewa Thamani Na Kipaumbele Kama Inavyostahili Kwa Mapana Na Ukubwa Wake. Sisi Kama #ROSTAM (Roma Na Stamina) Tunajaribu Kuonyesha Kuwa Hiki Ni Kiwanda Na Kinazalisha Na Kutoa Ajira Kwa Vijana Wengi Sana. Na Hii Ndiyo Sababu Iliyotupelekea Kuvaa Mavazi Haya Ya Kiwandani Tukiwa Jukwaani Tunaimba Parapanda. Bongo Flavour ni kiwanda kitoleeni macho tuiishi kauli mbiu ya Tanzania ya Viwanda.“wamesema ROSTAM.
Tazama picha na video za wawili hao walivyoitifua Mbagala.
https://youtu.be/YEB9Bpdxo7U
Mbagala jana zakhem
Wanaume aho, awanamda wa skendo na kuonesha mavazi ya bei Kali kesho yakifulia yana kwisha thamani,
Kazi kazi
Hatalii
Hapa kazi tu…..TZ ya viwanda
Ao jamaa wanatoa ujumbe throgh dresing but kam xhul ndogo aumwelew
Tanzania ya viwanda hiyo….😂😂😂
#yajayoyanafurahisha
Jamaa wabunifu sijawahi kuona….
Awana shobo
Hahhahahha umeua mkui
Wamepunguza bajet ya matumiz vyuma vimebana
nice boys