Burudani

Stamina, Roma kuja na albamu ya pamoja

Wakali wa muziki wa hip hop Bongo, Stamina na Roma wanakuja na albamu ya pamoja.

Stamina na Roma jukwaani

Aliyefichua hilo ni Stamina ambaye amesema kutokana na ukaribu wake na Roma wamegundua muziki wao unaendana hivyo wameamua kufanya albamu.

“Kuna albamu ya mimi na Roma imeshamalizika kurekodiwa kama unaona kuna picha tulikuwa studio kwa Manecky na wakina Ben Pol, wiki ile nyingine tunaachia single yetu ya pamoja,” ameiambia The Playlist ya Times Fm na kuongeza.

“Idea ya kufanya album pamoja tumegundua mimi na Roma tuna chemistry, kuanzia jukwaani, halafu apart ya kuwa hivyo ni mshikaji wangu mwingine kabisa, kwa siku nadhani yeye ndiye tupo pamoja kuliko mtu mwingine yeyote, basi tukasema na urafiki wetu tuuingize kwenye kazi ndio maana hata kwenye show tunafanya pamoja,” amesisitiza.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents