Burudani

Stamina: Treni ya Umeme Dar mpaka Moro ikikamilika,narudi kuishi zangu Moro

Leo April 12 Rais Dkt John Pombe Magufuli amezindua awamu ya kwanza ya ujenzi wa reli ambayo itakayorahisisha usafiri wa Dar es Salaam hadi Morogoro kwa njia ya treni.

Inawezekana mtu akawa anaishi Morogoro na kufanya kazi zake Da es Salaam kwani usafiri utakuwa wa uhakika na haraka zaidi. Rapper Stamina ambaye ni mzaliwa na Morogoro anayefanya mishe zake Dar, amehaidi kurudi kuishi Moro na wakati huo huo akiendelea kufanya mishe zake Dar endapo njia hiyo ya usafiri itaanza kufanya kazi.

“Ikikamilika hiyo Rais, naenda kuishi zangu Morogoro tu,” ameahidi Stamina wakati akipiga story na Prince Ramalove kupitia Kings Fm Leo.

Prince Ramalove
Kings Fm(Njombe)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents