Habari
Stereo kufanya collabo na Amani wa Kenya, ‘Kila Kitu’
Msanii wa Hip Hop Stereo aliye chini ya kampuni ya Unity Entertainment ya AY anatarajia kuachia ngoma yake mpya iitwayo Kila Kitu aliyomshirikisha msanii nyota kutoka Kenya Amani. Ngoma hiyo inafanyika Bongo Records.
Akiongea na Bongo5, Stereo amesema, “Mimi nimeshafanya nasubiri Amani na yeye halafu itatoka, mashabiki wakae mkao wa kula.”
Ameongeza kuwa ameona ni vyema kufanya muziki wenye mapana zaidi kwa kuwashirikisha wanamuziki wa nje ili kupanua soko la msanii kwasababu ya kuteka soko la kimataifa.