Siasa

Steve Nyerere atangaza kugombea Ubunge Iringa Mjini kwa Peter Msigwa – Video

Steve Nyerere atangaza kugombea Ubunge Iringa Mjini kwa Peter Msigwa - Video

Msanii wa Bongo Movie Steve Nyerere ametangaza rasmi kugombea Ubunge katika jimbo la Iringa mjini ambvalo mbunge wake na Peter Simon Msigwa.

Kupitia ukurasa wake wa Instgram Steve Nyerere ameandika ujumbe huu:-

“Nimekuwa nikipokea maombi kutoka Iringa, Vijana wenzangu, Baba na Mama zangu,Ndugu na Marafiki, hata Wasaniii wa Iringa, rasmi nitagombea Ubunge Iringa Mjini,ni haki yangu,narudi nyumbani, jumatano nitakuwa na kikao cha ndani na Vijana wa Iringa”

Hii inaelezwa kuwa huenda sababu ikiwa ni kauli ya Peter Simon Msigwa ya kusema au kumponda Waziri wa mlaiasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla kuwatumia wasanii wa Bongo Movie kutangaza Utalii kitendo ambacho ilipingwa vikali na wasanii wa Bongo movie ambapo Steve Nyerere alisema ni dharau.

https://www.instagram.com/p/B8Jm-AAh9Zk/

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents