Habari

Steve Nyerere na Irene Uwonya wakutwa na balaa lingine BASATA, Kosa la kuwarushia hela waandishi wa habari laachiwa BoT kulishugulikia (+Video)

Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limewataka waigizaji wawili wa filamu nchini Tanzania, Steve Nyerere na Irene Uwoya kujisajili haraka iwezekanavyo ili waweze kutambuliwa na baraza hilo.

Akiongea na waandishi wa habari leo Jumatano Julai 17, 2019 na kueleza kuwa wasanii hao walikuwa wanafanya kazi kiholela na kwa mazoea kwa muda mrefu.

Wakielezea kuhusu sakata lao la kuwarushia fedha waandishi wa habari, BASATA wamesema kuwa suala hilo halipo chini yao bali lipo chini ya Benki Kuu (BoT) na kuna sheria zao kuhusu mambo ya fedha.

Awali wasanii hao waliitwa kujieleza kuhusu tukio moja la kuwarushia fedha waandishi wa habari kwenye mkutano wao na waandishi.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents