Suarez aongeza tattoo ya shingo inayoonyesha style yake ya kubusu vidole ambayo huwa inawakilisha familia yake (+video)
Mara kadhaa nyota wa Barcelona, Luis Suarez amekuwa kionekana akibusu vidole vyake vya mikono pindi anaposhangilia wakati akipachika mabao.
Kupitia ushangiliaji wa staa huyo wazamani wa Liverpool ameamua kuchora ‘tattoo’ kwenye shingo yake huku akiandika jina la mtoto wake wa kike,Delfina.
Aina hiyo ya ushangiliaji wa Suarez hutimia baada ya kubusu kidole alichovikwa pete na mke wake, Sofia kisha kumalizia na vidole vitatu vikiwawakilisha watoto wake na mkewe ambayo ndiyo familia yake.
https://www.instagram.com/p/BrGMZVZA-0j/?utm_source=ig_embed&utm_campaign=embed_video_watch_again
Mchoro huo unakuja wakati huu ambao Barcelona ikiwa na kibarua cha kukabiliana na timu ya Espanyol hii leo siku ya Jumamosi katika La Liga.
Suarez amefunga jumla ya magoli tisa katika michezo 18 aliyoitumikia Barcelona msimu huu hivyo aina hiyo ya ushangiliaji imeoneka ikizaa matunda.