Picha
Sugu kesho kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa internet cafe ya Izzo B
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi aka Sugu kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa internet cafe ya rapper Emmanuel ‘Izzo B’ Simwinga.
Ofisi hiyo iitwayo Izzo Bizness Internet Cafe & Secretarial Bureau ipo TEKU University jijini Mbeya.Akiongea na Bongo5 Izzo amesema katika uzinduzi huo utakaoanza saa 8 mchana hakutakuwa na performance yoyote bali watafungua champagne za kutosha.
Pamoja na biashara hiyo, Izzo pia ana duka la nguo jijini humo.