Habari
Sumaye ashindwa uchaguzi ndani ya Chadema, licha ya kuwa mgombea pekee wa unyekiti Pwani
Aliyekuwa mgombea pekee wa nafasi ya uenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye ameshindwa kutetea nafasi hiyo baada ya kupigiwa kura ya hapana.
Katika uchaguzi huo uliofanyika jana Alhamisi Novemba 28, 2019 mjini Kibaha Mkoa wa Pwani, Sumaye aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania mwaka 1995 hadi 2005 amepigiwa kura 28 za ndio na 48 za hapana na kura moja imeharibika.
Inadaiwa kitendo cha kuchukua fomu za kuwania nafasi ya mwenyekiti wa Chadema ndiyo chanzo cha kushindwa kwenye uchaguzi mwenyekiti Kanda ya Pwani.
Chanzo Mwananchi