Michezo
Sunday Oliseh awa kocha mpya wa timu ya taifa ya Nigeria
Nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria, Sunday Oliseh ,40, ametangazwa na shirikisho la soka la nchi hiyo kuwa kocha mkuu wa timu hiyo kwa mkataba wa miaka mitatu. Oliseh amechukua nafasi ya Steven Keshi aliyetimuliwa.
Oliseh anakuwa mchezaji wa nne wa zamani wa Nigeria kupewa nafasi hiyo ya kocha mkuu wa timu ya taifa. Nigeria ipo kundi moja na Taifa Stars katika kuwania kucheza Kombe la Mataifa Afrika (AFCON)
Oliseh aliwahi kuvichezea vilabu vya Juventus, Italia, Ajax ya Uholanzi na Dortmund ya Ujerumani.