Burudani
Super Shine wafunika Navy Beach
Kiongozi wa kundi la muziki wa taarab la Super Shine, Salma Mbwana ‘Queen Salma’ amezitambulisha nyimbo mbili Red Card na tumewakata midomo na albamu ya Red Card katika bonaza la usiku wa Marafiki wa Ukweli na Familia
alisema albamu itakuwa na yimbo tano zikiwemo nyimbo hizo. Aidha amesema matarajio ya bendi hiyo ni kufanya uzinduzi wa albamu baada ya kuisha kwa mfungo wa ramadhani, mwaka huu .
“Katika utambulisho wetu ulienda salama, tukisindikizwa na Jokha Khasim, Hassan Alli, onyesho la kiduku na Khanga moja ndembe ndembe, nashukuru mungu lilienda vizuri” alisema.
Queen Salma aliongeza kwa kusema watakuwa wakifanya tamasha hilo kila jumapili, huku wakisindikizwa na Khanga Moja.