Michezo
Sweden yatinga robo fainali bila mkali wao Zlatan Ibrahimovic
Timu ya taifa ya Sweden imefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la dunia bila mshambuliaji wao hatari Zlatan Ibrahimovic baada ya kuifunga Switzerland bao 1 – 0.
Sweden ambayo mara kadhaa imekuwa na nyota wake hatari anayekipiga klabu ya LA Galaxy nchini Marekani, Zlatan Ibrahimovic safari hii imeshindwa kumjumuisha akutokana na umri wakekumtupa mkono na badala yake ikawaamini vijana wadogo.
Bao la Forsberg lililofungwa dakika ya 66 lilitosha kabisa kuipatia ushindi timu hiyo ya Sweden ambayo haikupewa nafasi kubwa ya kutinga hatua hiyo ya robo fainali.