Burudani
T.I. na mke wake wanadaiwa dola milioni 4.5 za kodi!
Rapper Clifford Harris, Jr aka T.I.anadaiwa zaidi ya dola milioni 4.5 zinazotokana na kushindwa kulipa kodi kuanzia 2012 hadi 2013.
Mtandao wa Page Six umedai kuwa mamlaka ya kodi nchini humo, IRS iliwasilisha nyaraka huko Georgia zikidai kuwa rapper huyo na mke wake Tameka “Tiny” Harris wanadaiwa kiasi hicho.
Hata hivyo haimaanishi kuwa rapper huyo amefulia bali mwaka 2006 alinunua nyumba yenye thamani ya dola milioni 4.26. Rapper huyo pia amekuwa akiishi maisha ya kifahari.