Michezo

Taarifa za usajili barani Ulaya Alhamisi hii, Hudson-Odoi, Paredes, Moses, Ramsey, Marcelo, Suarez, Sokoni

Kiungo Mhispania Denis Suarez, 25, atasalia klabuni Barcelona baada ya mipango ya kuhamia Arsenal mwezi huu kushindikana. (ESPN)

Liverpool inaminyana na Bayern Munich katika mbio za usajili wa winga wa Chelsea Callum Hudson-Odoi, 18. (Bild – in German)

Winga wa Chelsea na Nigeria Victor Moses, 28, anatarajiwa kwenda kwa mkopo klabu ya Fenerbahce mwishoni mwa msimu. (Goal)Paris St-Germain wanatarajiwa kuwapiku Chelsea katika usajili wa kiungo wa Zenit St Petersburg raia wa Argentina Leandro Paredes, 24. (Telegraph)


Mipango ya Arsenal ya kumuuza kiungo wao Aaron Ramsey, 28, kwenda Juventus inaonekana kuungwa mkono na kocha wa timu yake ya taifa ya Wales,Ryan Giggs, ambaye amedai kuwa mchezaji huyo atazidi kuboreka kwa kucheza kwenye timu kubwa kama Juventus. (Sky Sports)

Watford wana imani kuwa Kiungo wao Abdoulaye Doucoure, 26, atasalia klabuni hapo walau mpaka mwisho wa msimu huu, japo kumeshatangazwa dau la pauni milioni 50 na Paris St-Germain ambao wanataka kumsajili. (Evening Standard)

Beki wa Real Madrid defender Marcelo, 30, anataka kuungana na Cristiano Ronaldo katika klabu ya Juventus, na tayari ameshamweleza kocha wake juu ya dhamira yake hiyo: “Kama (Juventus) wateleta ofa ya kuninunua, itabidi tu mniruhusu niende”. (Marca via Tuttosport)

Newcastle wanajiandaa kusajili wachezaji wawili kwa mkopo kabla ya wiki hii kuisha. Tayari wameshawasilisha ofa kwa beki raia wa Italia anayechezea Monaco Antonio Barreca, 23, na winga wa Ureno anayekipiga na klabu ya Atletico Madrid Gelson Martins, 23. (Telegraph)

Chanzo BBC,

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents