Habari

Tahadhari yatolewa kwa watu wanaotaka kusafiri wiki hii kwa njia ya maji

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari kwa wananchi na wanaotumia usafiri wa majini kufuatia kuwapo kwa upepo mkali katika mikoa ya Tanga, Lindi, Mtwara, Dar Es Salaam, Mwanza, Kigoma, Rukwa, Ruvuma, Geita, Simiyu, Mbeya, Njombe pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Taarifa iliyotolewa jana usiku na kituo kikuu cha utabiri cha TMA imewataka watu wawe makini huku ikizitaka mamlaka zinazoshughulika na usafiri wa majini ziwe makini kwa kuchukua juu ya tahadhari  hiyo kwa kuhakikisha hakuna maafa yanayoweza kutokea.

Chanzo cha upepo huo mkali unaotarajiwa kuvuma kwa siku nne katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya  Hindi na maziwa yote makuu, Unatokana na kuimarika kwa hali ya hewa kwenye eneo la Kusini Mashariki mwa Bara la Afrika na mfumo wa upepo wa Kusini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents