Taifa Stars yaiangusha Tanzania na Rais Magufuli nchini Lesotho kwa kukubali kichapo
Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Tanzania, Taifa Stars imekubali kichapo cha goli 1-0 dhidi ya Lesotho kwenye mchezo wa kufuzu AFCON 2019.
Kwa matokeo hayo Taifa Stars inakuwa na alama 5 ikiwa imecheza michezo mitano jambo ambalo itahitajika kushinda dhidi ya Uganda kwenye mchezo wake wa mwisho huku ikiwaombea Cape Verde wenye alama 4 waitandike Lesotho.
Bado matumaini ni madogo kwa Taifa Stars kufuzu kwenda AFCON 2019. Mapema kabla ya mchezo huo Rais Magufuli aliwaomba vijana hao warudi nchini na ushindi lakini ndio hivyo mpaka dakika 90 wamekubali kichapo.
Vijana wangu – TAIFA STARS🇹🇿
Muda mfupi ujao nitakuwa nikitazama mchezo kati yenu na Timu ya Taifa ya Lesotho 🇱🇸.
Mimi na Watanzania wenzangu tunawatakia mchezo mwema, mrudi na ushindi.— Dr John Magufuli (@MagufuliJP) November 18, 2018
Kwa upande mwingine, Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo kabla ya mchezo huo alisema kuwa endapo Taifa Stars itafungwa basi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Harrison Mwakyembe ni vyema akajiuzulu.
https://twitter.com/zittokabwe/status/1064173327906979840