Habari
TAKUKURU yawaanika waliomuomba rushwa mfanyabiashara wa KariaKoo, kufikishwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) imesema kuwa imetekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mhe. John Pombe Magufuli yaliyotolewa Ijumaa Juni 7, 2019 wakati wa kikao kazi na Wafanyabiashara.
Kupitia akaunti ya Twitter ya Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbasi ameweka taarifa ambayo inaonyesha hatua ambazo zimeanza kuchukuliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU).
TAKUKURU yatekeleza Maagizo ya Rais Dkt. @MagufuliJP #TUNATEKELEZA2019#TanzaniaUpdates pic.twitter.com/bFFcz3mVS2
— Msemaji Mkuu wa Serikali (@TZMsemajiMkuu) June 10, 2019