Habari

Tamasha La Filamu NDIFF Kuzinduliwa Uganda Desemba 7

Things are looking ready and hot jijini Kampala na jinja this December as Organizers wa Nile Diaspora International Film Festival ambayo ni equivalent na tamasha la Kimataifa la Filamu kisiwani ZanzibarZiff, wametoa ratiba ya tamasha hilo la Filamu nchini humo.

Kwa mujibu wa taarifa ambayo bongo5.com imeipata tayari matayarisho yameshakamilika na kilichobaki ni kuanza kwa tamasha hilo siku ya tarehe 7 Desemba 2012 kwa sherehe za ufunguzi ambao imepewa jina la Nile Diaspora International Film Festival “Red Carpet Opening Night” ambayo imepangwa kufanyika katika Hoteli ya kimataifa Serena jijini Kampala.

Baadhi ya wageni walioalikwa ambao wamethibitishwa kwamba watakuwemo ni staa wa kike kutoka Ghana Nadia Buari, Staa wa kiume kutoka nchini Nigeria anayewakilisha Nollywood, Jim Iyke na Tonya Lee Williams wa Marekani kutoka kipindi cha Young and Restless, ambaye ni CEO wa Reelworld film festival ya Canada pamoja na msanii maarufu wa filamu za ‘Madea’ Tyler Perry kutoka Hollywood Marekani.

Baada ya ufunguzi huo, kutakuwa na semina ya watengenezaji wa filamu, ambayo itajumuisha wataalamu mbali mbali wa fani za filamu kama uandishi wa stori za filamu, mifumo ya uandaaji filamu kama upangaji wa bajeti na namna ya kuigiza stejini pamoja na filamu kutoka Africa Magharibi, Kusini, Mashariki, Ulaya na Marekani.

Baadhi ya mastaa ambao movie zao zitaonyeshwa ni pamoja na Mary j bilge, Malik Yoba, david Fernandez jr na Angela Basette.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents