Tamasha la Freestyle
Tamasha la kumtafuta makali wa Freestyle limemalizika salama kwa kutoa washindi watano, katika mkoa wa Dar es salaam ambao wataungana na washindi wengine kutoka mikoani ilikumtafuta mshindi wa Tanzania.
Katika tamasha hilo walijiunga watu mia moja, na kushindana na hatmaye wakapatikana watano ambao wamechaguliwa nafasi ya kuingia katika kinyang’anyiro hicho kwa kushindana na wengine.
Freestyle Battle ni mtindo wa kuimba kutokana na kile unachotakiwa kukiimba kwa wakati hupo, na wala si nyimbo uliyoiandika toka nyumbani, na ndiyo lengo la tamasha zima, kupata watu wenye uwezo wa kutoa mashairi ya hapo hapo.
Waamuazi katika shindano hilo, walikuwa Zavara aka Chief Rhymson na Fid Q, ambao walishirikiana na na wananchi ambao waliudhuria hapo, na ndiyo waliokuwa na nguvu kubwa katika maamuzi.
Mc akitoa mistari.
Mashabiki wakishangilia.
Mwanamuziki wa Hip Hop Mansu-Lee, Suka na Seba
Lusajo akishindana na mwenzake katika ni mtangazaji wa Clouds FM, Ncha kali ambaye alikuwa kama Mc wa Tamasha, akisaidiana na Fetty.
Wadau wa muziki wa Hip Hop wakisikiliza mashairi kwa kina.